Aliyekuwa mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali Edward Ouko amesema maisha yake yamo hatarini.
Ouko amesema japo maisha yake yalikuwa hatarini zaidi wakati alikuwa kazini, kwa sasa ndipo anahofia maisha yake zaidi.
Habari Nyingine: Mama amparura binti akiwasiliana na dume chooni

Akiongea na runinga ya Citizen Jumanne, Septemba 3, Ouko alisema ana wasiwasi sana kwa sababu waliokuwa wakimlenga wakati akiwa afisini huenda wakamsaka sasa.
"Nimekuwa nikiisha kwa hofu tangu nilipokuwa afisin, lakini kwa sasa ninahofia zaidi tangu nitoke afisini kwa sababu waliokuwa na nia mbaya wakati huo walijua nina ulinzi," alisema Ouko.Habari Nyingine: Mama awakosesha wakazi usingizi akidai anaonewa kijicho na wanawake kwa ploti
Ouko alisema familia yake pia imekuwa ikiisha kwa wasiwasi kutokana na vitisho kutoka kwa watu watajika.
Kwa wakati mmoja, Ouko alifichua, mkewe alihofia maisha yao na kumtaka awe mwangalifu katika kazi yake.

Ouko alisema bado ana walinzi wa serikali lakini ana wasiwasi kwani hajui atakuwa na wao mpaka lini.
"Bado nina walinzi wangu. Lakini sijui mpaka lini. Hakuna mpangilio wowote kuhusu usalama wa mkaguzii mkuu baada yake kuondoka afisini. Kunafaa kuwe na mikakati bora ya jinsi mtu kama huyo atapata usalama wake," alisema Ouko.Huku akikumbuka kazi yake kwenye afisi hiyo, ni swala la Eurobond ambalo lilikuwa moto sana kiasi cha kwamba Rais Uhuru Kenyatta mwenyewe alimkemea.
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia news@tuko.co.ke au WhatsApp: 0732482690.
Subscribe to watch new videosChanzo: TUKO.co.ke
ncG1vNJzZmijmajEorTIpaBnrKWgvG%2BvzmeinmdjZoF2fpNmpJqho52ubsXAp56uZamWurB5x5qrmqqZo7Zuu9SkpmaZo5q6onrHraSl